isasi wateja waliokuwa nje ya hoteli moja na mgahawa.
Eneo la katikati mwa jiji limezingirwa na maafisa wa jeshi na ubalozi wa Marekani mjini Ouagadougou umewatahadharisha raia wake wasiende eneo hilo.
Watu 30 waliuawa katika shambulio la kijihadi katika mgahawa mdogo ulio karibu na hapo Januari mwaka jana.
Kuna wasiwasi kwamba shambulio hilo huenda limetekelezwa na moja ya washirika wa mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda ambao bado wanaendesha shughuli zao katika eneo la Sahel, mwandishi wa BBC Alex Duval Smith amesema.
Waziri wa mawasiliano wa Burkina Faso Remis Dandjinou amesema haijabainika ni washambuliaji wangapi hasa waliohusika.
"Wamejibanza katika sehemu moja ya jumba waliloshambulia. Maafisa wa usalama wanaendesha oparesheni ya kuwafurusha," amesema kwenye televisheni.
Ufyatuaji wa risasi ulianza muda mfupi baada ya 21:00 (21:00 GMT) siku ya Jumapili katika barabara yenye shughuli nyingi ya Kwame Nkrumah.
Maeneo mawili, Hotel Bravia na Aziz Istanbul Restaurant, yanaonekana kulengwa na washambuliaji.
"Shambulio lilisababisha vifo vya watu 17, ambao uraia wake bado haujathibitishwa, na wanane wamejeruhiwa," taarifa ya serikali iliyonukuliwa na shirika la habari la AFP inasema.
Hospitali moja mjini humo ilisema mmoja wa waliouawa ni raia wa Uturuki.
Shambulio hilo linakaribiana sana na shambulio lililotekelezwa Januari 2016 ambapo watu wenye silaha walishambulia hoteli ya Splendid Hotel na mgahawa wa karibu wa Cappucino, pia katika barabara ya Kwame Nkrumah Avenue.
Watu zaidi ya 170 walishikwa mateka na 30 wakauawa.
Al-Qaeda walikiri kuhusika.
Burkina Faso inapatikana katika eneo la Sahel, ambalo linajumuisha pia nchi ya Mali ambapo makundi ya Kiislamu yamekuwa yakitekeleza mashambulio tangu mwaka 2012.
Sunday, 13 August 2017
Home
Unlabelled
Watu 17 wauawa katika shambulio mji wa Ouagadougou, Burkina Faso
Watu 17 wauawa katika shambulio mji wa Ouagadougou, Burkina Faso
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
No comments:
Post a Comment