Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee ma Watoto, Ummy Mwalimu ametoa wito kwa wanaume kupima saratani ya tezi dume huku akiwatoa hofu kuwa kipimo cha kupima saratani ya Tezi dume unapima kwa kutoa damu na sio kipimo kinachotembea mitandaoni.
Waziri Ummy ametoa wito huo mkoani Katavi Manispaa ya Mpanda pamoja na wananchi waliotoka wilaya ya Mlele na Tanganyika mara baada ya kuzindua zoezi la upimaji magonjwa ya sio ya kuambukizwa.
“Lakini inaweza kuwa wanaume mnaogopa kupima saratani ya tezi dume na mimi nitoe wito kwa wanaume mpime kwasababu pia sio kile kipimo kinachotembea mitandaoni kipo kipimo cha kupima saratani ya Tezi dume ambapo unapima kwa kutoa damu na sio vile mnavyofikiria kile kipimo ambacho watu wanakiogopa hicho sicho kipo kipimo rafiki,” aliongeza Waziri Ummy.
Hata hivyo Waziri Ummy alisema kuwa serikali itawachukulia hatua kali za kisheria watumishi wa afya wasiotoa huduma za kuridhisha na wenye kashfa ya kutokuwa na maadili ya kazi.
“Pale ambapo muuguzi amekujibi vibaya, daktari amekujibu vibaya na mkunga hajakufanyia vizuri, wauguzi wa hospitali ya Mpanda wengi ni wazuri tutajie jina na sisi tutamchukulia hatua na tutamwambia atupishe wapo watu wengi sana wanaotaka kufanya kazi katika hospitali za serikali,” alisema Ummy.
Friday, 18 August 2017
Home
Unlabelled
Ummy Mwalimu: Tezi dume inapimwa kwenye damu sio kile kipimo kinachotembea mtandaoni
Ummy Mwalimu: Tezi dume inapimwa kwenye damu sio kile kipimo kinachotembea mtandaoni
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment