Tff yaomba radhi kwa makosa ya maandishi kuhusu Ngao ya jamii - KULUNZI FIKRA

Thursday 24 August 2017

Tff yaomba radhi kwa makosa ya maandishi kuhusu Ngao ya jamii

 
 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, linaomba radhi wanafamilia wote wa mpira wa miguu kutokana na makosa ya maandishi yaliyoonekana kwenye utambulisho wa Ngao ya Jamii iliyotolewa Jumatano Agosti 23, 2017.

Ngao hiyo ilitolewa mara baada ya mchezo uliokutanisha timu za Simba SC na Yanga FC za Dar es salaam kwenye Uwanja wa Taifa jijini. Katika mchezo huo, Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 dhidi ya Yanga na kutwaa Ngao hiyo.

Watanzania hususani wanafamilia ya mpira wa miguu popote pale, TFF hatujapokea vizuri mwonekano wenye makosa kwenye Ngao hiyo ya Jamii kama ambavyo wadau hawajapokea vema suala hili.

Kutokana na makosa hayo, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, tayari amechukua hatua za kinidhamu kwa watumishi waliohusika kadhalika kuwasiliana na uongozi wa Simba SC kuirejesha Ngao hiyo ili kufanyiwa marekebisho yatakayobaki kwenye Kumbukumbu sahihi.

Hatutegemei tukio kama hili kujirudia tena.

No comments:

Post a Comment

Popular