Mkuu wa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani Fortunatus Musilimu, amefanya ziara ya kushtukiza kwenye kituo kikuu cha mabasi yanayofanya safari nje ya mkoa wa Mbeya na kufungia leseni za madereva saba kwa muda wa miezi sita.
Hatua ya kufungia leseni hizo imekuja baada ya kubainika kuwepo ukiukwaji wa sheria na taratibu za usalama barabarani, ikiwemo magari matano kubainika kuwa na mapungufu kwenye usukani pamoja na kufika kituo cha mwisho kabla ya muda halali uliopangwa.
Kamanda Musilimu alifika kituo hicho kilichopo jijini Mbeya mnamo saa 11, alfajiri na kisha kuanza ukaguzi.
Katika ukaguzi huo pia magari hayo matano yalibainika kuwa na uppungufu kwenye magurudumu, kitu ambacho kilimsukuma kamanda huyo kuyazuia kuendelea na safari zake.
Utekelezaji wa zoezi hilo unatajwa kuwa na lengo la kupunguza ajali za barabarani zinazoonekana kukithiri nchini Tanzania.
Kitendo cha kufanya ziara hiyo ya kushtukiza, kinaweza kufananishwa na nyendo za rais John Magufuli, ambaye mara kadhaa ameshuhudiwa akifanya ziara katika ofisi mbalimbali za umma, pasi na kutoa taarifa.
Saturday, 19 August 2017
Home
Unlabelled
Mrithi wa Mpinga afuata nyayo za Magufuli
Mrithi wa Mpinga afuata nyayo za Magufuli
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment