RC Anna Mghwira awaongoza wakazi wa Kilimanjaro kuwapokea wanafunzi watatu wa shule ya Lucky Vincent waliowasili asubuhi kutoka Marekani.
Wanafunzi watatu wa Shule ya Lucky Vincent waliokuwa wakipatiwa matibabu Marekani wamewasili nchini asubuhi hii katika Uwanja wa KIA.
Kwa mujibu wa mh. Lazaro Nyalandu ndege hii kubwa imekuja na vifaa tiba ambavyo vitasambazwa katika hospitali za serikali na binafsi.
Furaha imetawala ujio wa watoto watatu wa Shule ya Lucky Vicent waliowasili leo Ijumaa, Agosti 18 wakitokea nchini Marekani kwenye matibabu baada ya kupata ajali Mei mwaka huu.
Wazazi na ndugu waliruhusiwa kuingia ndani ya ndege hiyo kuwapokea watoto wao ambao wamepata nafuu kwa kiasi kikubwa.
Wilson Tarimo alikuwa wa kwanza kushuka katika ndege akiambatana na mdogo wake aliyeingia katika ndege kwa ajili ya kumpokea.
Baada ya hapo aliyefuatia ni Saidia Awadhi pili akifuatana na Doreen Mshana kushuka katika ndege hiyo iliyokuwa na wajumbe 16 ambao waliambatana na watoto hao.
Baada ya kushuka walipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira aliyeambata na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Arusha.
Watoto hao wote wakati wanashuka walionekana wenye nyuso za furaha baada ya kukaa Marekani kwa miezi mitatu wakipata matibabu.
Friday, 18 August 2017
Home
Unlabelled
Manusura wa ajali ya ya wanafunzi wa Lucky Vincent wawasili,walakiwa na RC wa Kilimanjaro
Manusura wa ajali ya ya wanafunzi wa Lucky Vincent wawasili,walakiwa na RC wa Kilimanjaro
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment