Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Simba, Juma Liuzio amefichua kwamba hana presha kabisa katika kikosi hicho na ndiyo maana ametulia na kuanza vizuri msimu.
Liuzio ambaye aliifungia Simba bao moja katika ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting wikiendi iliyopita, alisema anafurahi kuanza vizuri msimu na anatazama mbele kufanya makubwa.
"Mashabiki wengi hawana matarajio makubwa kwangu, hii inanisaidia kutuliza akili na kufanya vizuri tofauti na wengine," alisema Liuzio.
Akizungumzia upande wa washambuliaji, Liuzio alisema wako vizuri kwa sasa lakini wanahitaji muda zaidi kuweza kutisha zaidi.
"Bado tuna changamoto ya kufanya vizuri, wachezaji wengi ni wapya na wanajipanga kuisaidia timu, kocha bado ana kazi ya kutuunganisha," alisema.
Thursday 31 August 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment