Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Simba, Juma Liuzio amefichua kwamba hana presha kabisa katika kikosi hicho na ndiyo maana ametulia na kuanza vizuri msimu.
Liuzio ambaye aliifungia Simba bao moja katika ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting wikiendi iliyopita, alisema anafurahi kuanza vizuri msimu na anatazama mbele kufanya makubwa.
"Mashabiki wengi hawana matarajio makubwa kwangu, hii inanisaidia kutuliza akili na kufanya vizuri tofauti na wengine," alisema Liuzio.
Akizungumzia upande wa washambuliaji, Liuzio alisema wako vizuri kwa sasa lakini wanahitaji muda zaidi kuweza kutisha zaidi.
"Bado tuna changamoto ya kufanya vizuri, wachezaji wengi ni wapya na wanajipanga kuisaidia timu, kocha bado ana kazi ya kutuunganisha," alisema.
Thursday, 31 August 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
No comments:
Post a Comment