Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema CUF sana Katibu mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad kwa kudhani kuwa kama angepata yeye basi wamepata wote kumbe ni tofauti kitu ambacho waliwakosea Wazanzibar.
Profesa Lipumba ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua kikao cha kwanza cha kawaida cha Baraza Kuu la Uongozi la CUF kilichofanyika katika makao makuu ya chama hicho, maeneo ya Buguruni jijini Dar es Salaam.
Ameongeza kuwa hali ya kumdekeza Maalim Seif imesababisha CUF kushindwa kupata viongozi watakaoingia katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na kutokuwepo kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
“CUF tumemdekeza kwa muda mrefu na zile nyimbo tulizokuwa tukiimba ya kuwa akipata Seif tumepata sote zilikuwa zimemuingia kichwani kwelikweli na yeye alitafsiri kuwa akikosa Seif tumekosa sote",amesema Profesa Lipumba.
"Matokea yake tumekosa kuwa na uwakilishi katika Baraza la Uwakilishi jambo ambalo limetuathiri kisiasa hasa Zanzibar. Hili kosa kubwa tuliowakosea Wazanzibari” amesema Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua kikao cha kwanza cha kawaida cha Baraza Kuu la Uongozi la CUF kilichofanyika katika makao makuu ya chama hicho, maeneo ya Buguruni jijini Dar es Salaam.
Ameongeza kuwa hali ya kumdekeza Maalim Seif imesababisha CUF kushindwa kupata viongozi watakaoingia katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na kutokuwepo kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
“CUF tumemdekeza kwa muda mrefu na zile nyimbo tulizokuwa tukiimba ya kuwa akipata Seif tumepata sote zilikuwa zimemuingia kichwani kwelikweli na yeye alitafsiri kuwa akikosa Seif tumekosa sote",amesema Profesa Lipumba.
"Matokea yake tumekosa kuwa na uwakilishi katika Baraza la Uwakilishi jambo ambalo limetuathiri kisiasa hasa Zanzibar. Hili kosa kubwa tuliowakosea Wazanzibari” amesema Profesa Lipumba.

No comments:
Post a Comment