Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, mchungaji Peter Msigwa, amesema upo umuhimu wa kuongeza mshahara kwa madiwani waliopo nchini kutokana na kazi kubwa wanayoifanya viongozi hao.
Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio Jana Jumatano Oktoba 4, kiongozi huyo ametolea mfano kwenye Halmashauri ya Iringa Mjini, kwa kusema madiwani wa eneo hilo hulipwa shilingi 40,000 kwa kila kikao kimoja na nauli shilingi 10,000.
“Madiwani wanafanya kazi kubwa sana na ukiangalia kiinua mgongo chao baada ya miaka mitano, hakizidi milioni 12,”
Msigwa amebainisha mshahara anaolipwa diwani kwa kila mwezi kuwa ni shilingi 350,000 na kuongeza kuwa kuna utofauti wa malipo ya posho kwa viongozi hao wa kata, kutokana na makusanyo yanayopatikana kwenye halmashauri husika.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano mkuu wa 33, wa Jumuia ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT), jana Jumanne, rais John Magufuli, amesema hatoongeza mishahara, huku akiwataka madiwani wasiokuwa na vyanzo vya kipato, wajiuzulu.
“Na ndiyo maana mimi mishahara waliokuwa wanapata wengine sikupandisha na sitapandisha, kwa sababu ninawajibu wa kuwatumikia watanzania kwanza, na kazi ya udiwani masharti tunapojaza fomu, tunaambiwa lazima uwe na kazi maalum inayokupa kipato,” alisema kiongozi huyo.
“Sasa kama wapo madiwani waliojaza hiyo nafasi na hawana kazi ya kuwapa kipato, ni afadhali wajiuzulu udiwani” aliongeza Dkt. Magufuli.
Wednesday, 4 October 2017
Home
Unlabelled
Mbunge Peter Msigwa alilia ongezeko mshahara kwa madiwani
Mbunge Peter Msigwa alilia ongezeko mshahara kwa madiwani
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment