Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Hamphrey Polepole amesema mchakato wa Katiba ulikwama kwa sababu hakukuwa na uelewa wa pamoja nini wananchi wanataka jambo ambalo, tayari limeshaeleweka ndani ya chama hicho.
Akizungumza leo Alhamisi katika kipindi cha Maisha Mseto kinachorushwa na redio Times FM, Polepole amesema yeye ni muumini wa maoni ya wananchi kwenye mchakato wa Katiba mpya.
Amesema wakati ya mchakato wa Katiba mpya alikuwa miongoni mwa wajumbe waliokusanya maoni ya wananchi ataendelea kuunga mkono maoni yao.
“Nilikusanya maoni ya wananchi nchi nzima ya Tanzania na ninajua nini Watanzania wanasema kwa hiyo, mimi ni muumini wa maoni ya wananchi,” amesema.
Amesema mchakato huo ulikwama kwa sababu hakukuwepo na uelewa wa nini Watanzania wanataka.
Hata hivyo alidai kuwa mabadiliko makubwa yanayofanywa ndani ya chama hicho yanaakisi kushughulikia kero za wananchi.
“Siasa safi ni kushughulika na kero za wananchi wetu, chama kimejitathmini na kujisahihisha kwa sababu tumepata usahidi kwamba kuna mahali tulikosea kwa hiyo, tunao utaratibu wa kujikosoa,” amesema.
Polepole amesema uongozi wa Rais John Magufuli umejikita zaidi katika kushughulikia kero za wananchi kwa kuhakikisha watumishi wa umma wanafanya kazi kwa uadilifu huku wakiweka mbele maslahi ya Taifa.
pole.jpg
Thursday, 12 October 2017
Home
Unlabelled
Dar es salaam: Polepole ataja sababu zilizokwamisha mchakato wa katiba mpya
Dar es salaam: Polepole ataja sababu zilizokwamisha mchakato wa katiba mpya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...

No comments:
Post a Comment