Mtuhumiwa mmoja aliyeshiriki kununua madiwani wa CHADEMA Meru amejisalimisha kwa mganga wa kienyeji ili kulinda kibarua chake kisiweze kuota nyasi kufuatia uchunguzi mbalimbali ambao unaendelea.
Mbunge wa Jimbo la Arumeri Mashariki, Joshua Nassari amethibitisha hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anaishi maeneo ya Mukidoma Usa- River na kudai kuwa tayari anao ukweli wote kuhusu hilo na kuahidi kuutoa muda si mrefu.
"Mmoja wa watuhumiwa wa rushwa ya ununuzi wa madiwani Meru aishie maeneo ya Mukidoma Usa-River ameleta mganga toka kanda ya ziwa, na yupo nyumbani kwake . Lengo ni kumsaidia mtuhumiwa huyu asipoteze ajira yake. Mganga huyu ameletwa na mama wa mtuhumiwa. Tutaanika hadharani acha tuone tofauti ya Mungu na miungu" aliandika Joshua Nassari
Mbunge wa Jimbo la Arumeri Mashariki, Joshua Nassari siku kadhaa zilizopita aliachia ukweli juu ya wateule wa Rais John Pombe Magufuli jinsi ambavyo walikuwa wakipanga mipango ya kununa madiwani wa CHADEMA na baadaye alichukua ushahidi huo na kuupeleka TAKUKURU.
Thursday, 12 October 2017
Home
Unlabelled
Arusha: Aliyeshiliki kununua madiwani wa chadema akimbilia kwa mganga
Arusha: Aliyeshiliki kununua madiwani wa chadema akimbilia kwa mganga
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...

No comments:
Post a Comment