Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amefunguka na kusema kwa sasa ametimiza wajibu wake kukutana na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na kuweza kutoa sababu zake kwanini anaamini Bunge linatumiwa na serikali na kuwa ni bunge lisilo na meno.
Zitto Kabwe ambaye jana aliweza kukutana na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na kufanya mahojiano nao amesema kuwa kwa upande wake yeye ametimiza wajibu wake hivyo sasa kazi imebaki kwenye Kamati husika kupima maelezo yake na kile anachotuhumiwa na kufanya maamuzi, lakini pia amesema anaamini Kamati hiyo itafanya maamuzi kwa haki na bila ya kuwa na woga wala hofu.
"Nipo huru baada ya masaa 24 tangu nikamatwe na polisi Uwanja wa Ndege Dar es Salaam na kuletwa Dodoma kwa gari. Nimekutana na Kamati ya Bunge ya Kinga na Haki na kuhojiwa. Nimetoa maelezo yangu yenye lengo la kulinda Uhuru wa maoni na kulinda hadhi ya Bunge kama mhimili wa dola dhidi ya kuingiliwa na Serikali. Nimetimiza wajibu wangu. Mpira sasa upo kwenye Kamati natumai wataamua kwa haki na bila woga na hofu" alisema Zitto Kabwe
Zitto Kabwe alikamatwa na jeshi la polisi kwa amri ya Katibu wa Bunge Dr. Thomas D. Kashililah na kuweza kusafirishwa kutoka Dar es Salaam mbaka Dodoma chini ya ulinzi wa jeshi la polisi kwa lengo la kuhojiwa na kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kutokana na kauli zake alizowahi kutoa kupitia mitandao ya kijamii dhidi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai na Bunge.
Friday, 22 September 2017
Home
Unlabelled
Zitto kabwe: Nimetimiza wajibu wangu
Zitto kabwe: Nimetimiza wajibu wangu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment