STRAIKA wa Simba, Emmanuel Okwi, amesema hakuweza kufanya vizuri katika mchezo dhidi ya Mbao FC, kwani mabeki wa wapinzani wao hao walimkamia kupita kiasi.
Okwi hakuweza kufurukuta dhidi ya Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa juzi Alhamisi kwani alitulizwa kwa kuchezewa rafu mara 12.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao iliilazimisha Simba sare ya mabao 2-2 na kuwa timu ya kwanza kutikisa nyavu za Wekundu wa Msimbazi msimu huu.
Okwi, mwenye mabao sita katika ligi kuu akiwa kinara wa ufungaji, alishindwa kufunga kutokana na mabeki wa Mbao kuwa makini wakiongozwa na Boniface Maganga na Yusuph Mgeta.
Kwa pamoja na wachezaji wengine wa Mbao, mabeki hao walimchezea Okwi raia wa Uganda faulo 12 katika muda wote wa dakika 90 za mchezo huo.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Okwi alisema Mbao walimkamia kupita kiasi ndiyo maana alishindwa kufunga: “Mbao walikamia sana aisee kwani mabeki wao walikuwa wakinikaba hadi kivuli.
“Nilijitahidi kutumia mbinu zangu lakini imekuwa ngumu kweli lakini tunashukuru Mungu kwa sare hii kwani tangu msimu uliopita nilisikia Mbao inaisumbua sana Simba.”
Hata hivyo, mwamuzi aliyechezesha mchezo huo, Athuman Lazi aliwapa kadi za njano baadhi ya wachezaji wa Mbao kwa kucheza mchezo usiofaa kwa wachezaji wa Simba akiwemo Okwi.
Saturday, 23 September 2017
Home
Unlabelled
Okwi: Mbao sio wa mchezo mchezo
Okwi: Mbao sio wa mchezo mchezo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment