Lissu kufanyiwa upasuaji mwingine kesho - KULUNZI FIKRA

Saturday, 23 September 2017

Lissu kufanyiwa upasuaji mwingine kesho

Wakati Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki (chadema) Tundu Lissu kesho  anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwingine, fedha zilizochangwa na wabunge hatimaye  mchana zimeonekana katika akaunti ya hospitali ya Nairobi.

Lissu ambaye tangu Septemba 7 amekuwa akipatiwa matibabu,katika hospitali hii kesho  atafanyiwa upasuaji tena na jopo la madaktari kutazama athari zaidi katika mwili wake.

Akizungumza na kulunzifikra blog mmoja wa wauguzi wa hospitali ya Nairobi, ambaye ameomba kuhifadhiwa jina, amesema upasuaji unahusu eneo la nyonga.

No comments:

Post a Comment

Popular