Mwili wa mtoto mchanga anayekadiriwa kuwa na umri wa siku 1, ameokotwa katika mtaro wa maji machafu huko Unga Limited
Mwili wa kichanga waokotwa ukiwa umetupwa kwenye mfereji wa maji machafu jijini Arusha
Kichanga kinachokadiriwa kuwa na umri wa siku moja kimeokotwa kikiwa kimefariki na kutelekezwa kwenye mfereji wa kupitisha maji machafu katika eneo la mtaa wa Ali Nyanya kata ya Ungalimited jijini Arusha.
Kulunzifikra blog imefika eneo la tukio hilo ambalo wakazi wake wengi wanajishughulisha na biashara ndogondogo na hapa baadhi ya mashuhuda wanaelezea mazingira ya kichanga hicho kupatikana huku wakilaani kitendo hicho.
Omari Shehe ni mwenyekiti wa mtaa huo ambaye anakemea vitendo hivyo na kuahidi kusaidia vyombo vya dola kumtafuta mhusika ili iwe fundisho kwa wengine wenye nia ovu kama hiyo.
Vitendo vya utelekezaji na utupaji wa watoto vimeendelea kuota mizizi katika maeneo mengi hususani ya mjini sababu kubwa ikielezwa kuwa ni kile kinachodhaniwa ni baadhi ya wanaume kukataa majukumu lakini pia kupungua kwa maadili ndani ya jamii.
Monday, 11 September 2017
Home
Unlabelled
Arusha: Mtoto mchanga aokotwa kwenye mfereji wa maji machafu akiwa amefariki
Arusha: Mtoto mchanga aokotwa kwenye mfereji wa maji machafu akiwa amefariki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment