Tarime: kamanda wa polisi ashindwa kueleza sheria iliyovunjwa na Esther Bulaya kwenda jimbo lisilo lake - KULUNZI FIKRA

Tuesday 22 August 2017

Tarime: kamanda wa polisi ashindwa kueleza sheria iliyovunjwa na Esther Bulaya kwenda jimbo lisilo lake

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya ashindwa kueleza kifungu cha sheria au kununi ya adhabu aliyovunja Esther Bulaya.

Wiki iliyoisha Esther Bulaya ambaye ni mbungewa Bunda mjini, aliwekwa Korokoroni kwa kile kilichodaiwa ni kufanya mkutano wa hadhara kwenye jimbo lisilo lake la Tarime Vijijini.

Bulaya ambaye ni CHADEMA, alienda kwenye jimbo la Heche la Tarime vijijini ambaye pia ni CHADEMA. Heche alikuwa na Ziara jimboni mwake ambapo kulifanyika mkutano Nyamongo, Walikuwa na mkutano wa hadhara, Polisi hawakufurahishwa na kitendo cha Bulaya kupanda jukwaani kusalimia na kuhutubia kwani sio jimboni kwake.

No comments:

Post a Comment

Popular