Dar es Salaam. Imebainika kwamba pamoja na uwepo wa sheria ya makosa ya mtandao lugha ya matusi imeendelea kutumika huku mkoa wa Dar es Salaam ukiwa kinara.
Pia Mkoa wa Mwanza nao umebainika kuwa kinara kwa upande wa makosa ya wizi fedha mtandaoni ukilinganisha na mikoa mingine.
Takwimu zilizotolewa na jeshi la polisi zimeonyesha kuwa jumla ya matukio 327 ya matusi mtandaoni yameripotiwa kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu.
Msemaji wa Jeshi hilo ACP Barnaba Mwakalukwa amesema matukio mengi ya makosa ya matusi yanatokea wilaya ya Temeke.
Hata hivyo Mwakalukwa amesema takwimu hizo inaonyesha kupungua ikilinganishwa na mwaka jana ambapo matukio kama hayo 911 yaliripotiwa na wilaya ya Kinondoni iliongoza.
"Jumla ya matukio 1663 ya wizi wa fedha kwa njia ya mtandao zimeripotiwa huku mkoa wa Mwanza ukionekana kuwa kinara ikifuatiwa na Ilala na Kinondoni.
"Unaweza kuuliza kwa nini Mwanza, ule mji umekua kuna wafanyabiashara wakubwa, wahalifu nao wanabuni mbinu mpya," amesema
Amesema jumla ya watuhumiwa 315 walikamatwa kuhusiana na makosa ya uhalifu mtandaoni na kesi 153 zimefikishwa mahakamani.
Kati ya kesi hizo wahusika katika kesi 19 walikutwa na hatia na nyingine zipo chini ya upelelezi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi na Mawasiliano ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Hamza Hassan amesema ipo haja ya kuendelewa kutolewa elimu kuhusu sheria ya mtandao ili kupunguza vitendo vya ukiukwaji maadili.
"Unaweza kufanya jambo leo mtandaoni halafu athari zake zikaanza kuonekana baada ya miaka kadhaa, tuitumie vyema mitandao na elimu zaidi itolewe,"
Hassan akiwa na kamati yake wametembelea Mamlaka ya Mawasiliano TCRA na kupewa semina kuhusu sheria ya makosa ya mtandao.
Thursday, 24 August 2017
Home
Unlabelled
Dar kinara wa matusi,Mwanza wizi
Dar kinara wa matusi,Mwanza wizi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment