Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limepiga marufuku madereva pikipiki maarufu bodaboda kuwapakia watoto wenye umri chini ya miaka tisa
Dereva yeyote atakayekiuka agizo hilo atakamatwa na kufunguliwa kesi mahakamani ambapo anaweza kuhukumiwa kwenda jela au kulipa faini kulingana na hakimu atakanyoamua
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kipindi cha 'Bodaboda' ambacho kitaonyeshwa kwenye televisheni ya Clouds, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi, ACP Theopista Malya, alisema kuna tabia ya madereva wa pikipiki kukodishwa kuwapeleka watoto wadogo shule jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
"katika mambo ambayo sheria za usalama barabarani zinazomwongoza dereva wa bodaboda mojawapo ni kupakia watoto wenye umri chini ya miaka tisa. Unakuta anabeba watoto wanne kwenye pikipiki moja na mwingine mdogo yupo mbele yake.
"Licha ya kwamba ni kosa kisheria lakini pia ina athari kubwa sana kwa usalama wa mtoto mdogo kwani upepo unampiga kwa kasi hivyo hawezi kustahimili hali hiyo mwishowe anapata magonjwa", alisema ACP Malya.
Kuhusu elimu kwa madereva hao, bosi huyo wa kikosi cha usalama barabarani alisema polisi kwa kushirikiana na kamati ya usalama barabarani nchini wameweka mikakati ya kupunguza ajali ikiwa ni pamoja na kuongeza kiwango cha utoaji elimu kwa waendesha bodaboda.
Tuesday, 15 August 2017
Home
Unlabelled
Bodaboda marufuku kupakia watoto mwenye umri wa nchini ya miaka tisa
Bodaboda marufuku kupakia watoto mwenye umri wa nchini ya miaka tisa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
No comments:
Post a Comment